Monday 17 September 2018

🌹ADABU YA MUME KWA MKEWE.🌹


Usitangaze udhaifu wa mkeo kwa familia na marafiki, kila mmoja anamtunzia mwenziwe hadhi yake.

Usiwe na mtizamo mbaya wala kuzungumza naye kwa hisia kali huwezi kujua atatafsiri vipi.!!

Usimlinganishe mkeo na wanawake wengine, huwezi kujua hao wanawake wengine wanapitia hali gani kimaisha, kila mwanamke anasifa zake.

Usisahau kwamba ni mkeo umemuoa, yeye si kijakazi, muhudumie kama malikia na atauonyesha ulimwengu kwamba Mumewe ni mfalme na utamtawala maishani.

Mpe kipaumbele na ni wajibu wako binafsi kumfanyia jambo na sio watuwengine.

Usimlaumu mbele za watu hata kama kakosea, mlinde, muhimize, mrekebishe faraghani, ukifanya hivyo kamwe hatokusahau.

Usimnyime huduma za kitandani kwa kujifanya mgonjwa/kuchoka ama kutokuwa na hamu, kumbuka wanaume wengine wanatafuta nafasi hiyo.

Usimlinganishe mkeo na mtalaka wako ama mkeo aliyefariki maana wewe ni mume wa pekee kwake.

Usimkemee wala kumkosoa mbele ya watoto, ni malezi mabaya kwa watoto maana wewe ni mwalimu wao, wanakutazama wewe japo unadhani ni watoto tu!!.

Mtazame mkeo kama kavaa vizuri kabla hajatoka maana akipendeza yeye na wewe unaheshimika na ukipendeza wewe yeye anaheshimika.

Usikubali marafiki kuwa karibu na mkeo, weka mipaka maana hujui nia zao.

Usitoke kuoga na haraka haraka ukavaa nguo ukatoka pasi yeye kukukagua, mkeo kazungukwa na wanaume wanadhifu wanaojali mavazi na utanashati.

Wazazi, ukoo na marafiki sio waamuzi kwa mambo ya mkeo, usipoteze muda kutafuta uamuzi wa mwisho kutoka kwao, ithibiti ndoa yako.

Mapenzi yako yasiwe kwa sababu ya mazingira au kihali hata kama ulimuoa kwa misingi hiyo kwa sasa ni mkeo mpende bila masharti, hali uweza kubadilika na ikiwa ndio msingi basi ndoa itavunjika.

Mkeo anahitaji umakinike kwake na umsikilize kama mtoto, usiwe mkali msikilize kwa makini na atakupenda.

Usijilinganishe na mkeo, yeye ni mke kwa hivyo msaidie tu maanandoa ni kusaidia.

Usimuhukumu mkeo, ni msaidizi wako na kiumbe dhaifu mchukulie kwa mtazamo huo na utapata utulivu wa akili.

Mume mzembe hajali, haogi, jiweke nadhifu ukiwa na yeye nukia vizuri, harufu mbaya inamkirihisha ila hawezi kukwambia.

Usiwe na urafiki na waume walio na mtazamo mbaya kuhusu ndoa. Watakuharibu mawazo.

Mkeo ana thamani kubwa sana ndio maaana ukatoa vitu vya thamani kumuoa, penzi lenu lifanye jipya, uzembe haufai.

Kuzaa ni majaaliwa, mpende mkeo awe na watoto au asiwe nao, usiwabague watoto kwa jinsia wafunze dini na watakuwa wacha Mungu hadi maishani mwao.

Hauwi mzee kwa mkeo katika kumburudisha, usiwe na ugomvi naye mutakuwa katika kheri, usiwache kuwajali watoto wako na mkeo kwa sababu ya wanawake wengine au sababu yoyote ile, wao ni wewe na wewe ni wao.

Mume anayedumu na ibada ana usalama, omba kila siku, muombee mkeo na watoto.

Ukijiunga na group letu la UISLAMU CHAGUO LANGU na kulike page yetu ya Habari za kiislamu na kututembelea Furaha ya Ndoa utaelimika na ndoa yako.

💕TUKIYAFANYA HAYA TUTAKUWA NA NDOA BORA MNO!!💕

JINSI YA KUMFURAHISHA MKEO

Ili kusaidia familia za Kiislam na kueneza mafundisho ya Uislam katika kujenga familia, MSA (Muslim Students Association) katika Chuo Kikuu cha Alberta, Canada, kimetayarisha ufupisho wa tafsiri ya vitabu viwili. Vitabu katika lugha ya kiarabu vilivyotungwa na Shaykh Muhammad 'Abdul-Haliym Haamid. Mwanachuoni wa Kimisri, ambaye amemaliza masomo yake katika chuo cha Islamic University cha Madiyna An-Nabiwiyyah huko Saudi Arabia. Vitabu vyenyewe ni :
1.    Namna ya kumfurahisha Mkeo
2.    Namna ya kumfurahisha Mumeo
Hivi ni vitabu vizuri kabisa vya Kiarabu ambavyo tumeviona
katika somo hili. Vimekwenda mbali katika kuelezea, kuanzia
haki na wajibu mpaka adaab (tabia njema) na kwenda mbali
katika kutekeleza haki hizi katika maisha ya kila siku. Ufupisho ufuatao unamulika zaidi katika majukumu  ya nini kinaweza au kinachotakiwa kifanywe. Kila jambo lililotajwa na muandishi limeegemezwa katika ushahidi wa Qur-aan, Sunnah au matendo ya Maswahaba, bali ushahidi haukuwekwa katika tafsiri hii. Ifuatayo ni tafsiri ya kitabu cha kwanza.
Usisite kuituma kwa wengine au kuitoa kopi kwa njia nyoyote, ilimradi tu hutofanya mabadiliko yoyote, au kuongeza, au kupunguza bila ya ruhusa.
Ifuatayo ni sehemu ya KWANZA ya ufupisho wa kitabu “ How to make your wife happy” na Shaykh Muhammad 'Abdul-Haliym Haamid.

1.    Mapokezi Mazuri
Baada ya kurudi kutoka kazini, skuli, safarini, au popote pale palipowatenganisheni: 
·         Anza kwa maamkizi mazuri
·         Anza kwa Assalaamu 'Alaykum na tabasamu.
·         Salaam ni Sunnah na ni duaa kwake (mkeo) pia.
·         Mpe mkono na ziache habari mbaya mpaka baadae.



2.       Maneno mazuri na makaribisho ya kufurahisha
·          Chagua maneno mema na jiepushe na maneno mabaya.
·          Shughulika nae unaposema au anaposema yeye
·         ·Sema kwa ufasaha na rejea maneno inapohitajika mpaka  afahamu/aelewe.
·          Mwite kwa majina mazuri anayoyapenda, mfano Mpenzi wangu, honey (asali, tamtam),  (habibty),  swaaliha (mwanamke mwema), n.k



3.       Urafiki na maliwazo
·          Tumia muda kuzungumza nae
·          Mfikishie habari njema
·          Kumbuka kumbukumbu  zenu  nzuri za kuwa  pamoja. 


       
4.       Michezo na burudani 
·         Mfanyie mzaha na jiweke katika hali ya furaha
·         Chezeni na mshindane katika michezo na mambo mengine.    
·         Mchukue kuangalia aina za burudani zilizo halali.
·         Jiepushe na mambo ya haram katika kuchagua aina ya burdani.


5.                  Msaada katika kazi za nyumbani
              ·         Fanya kile ambayo wewe mwenyewe unaweza/ unapenda kukifanya ili kumsaidia, hasa anapokuwa mgonjwa au amechoka.
·         La muhimu kuliko yote ni kumuonyesha wazi kuwa unathamini/unashukuru jitihada zake katika kazi.


6.                  Kushauriana (Shuura)


·          Hususan katika masuala ya familia
·          Kumpa hisia kuwa maoni yake ni muhimu kwako.
·         Kuyazingatia maoni yake kwa makini
·         Kuwa tayari kubadilisha maoni yako kwa maoni yake iwapo yatakuwa ni bora zaidi.
·         Mpe shukurani kwa msaada wake wa maoni.


7.                  Kutembelea wengine


·         Chagua watu wenye malezi mema wa kufanya mahusiano nao. Kuna malipo makubwa katika kuwatembelea jamaa na watu wacha Mungu. (Sio kuwatembelea kwa kupoteza wakati)
·         Kuwa muangalifu kuhakikisha tabia za Kiislamu wakati mnapowatembelea watu.
·         Usimlazimishe kuwatembelea wale ambao yeye hajisikii raha kuwa nao.


8.                  Muongozo wakati wa kusafiri


·         Muage vizuri na kumpa ushauri mwema
·         Mtake akuombee dua
·         Watake jamaa wacha Mungu na marafiki kuiangalia familia wakati wa kutokuwepo kwako.
·         Mpe pesa za kutosha kwa mahitaji anayoweza kuhitajia
·         Jaribu kuwa na mawasiliano nae ama kwa simu, e-mail (barua pepe), barua, n.k.
·          Rejea haraka iwezekanavyo.
·         Mchukulie zawadi
·         Jiepushe na kurejea nyakati zisizotarajiwa au nyakati za usiku.
·         Mchukue (safarini) ikiwezekana.


9.                  Msaada wa kifedha


·         Unatakiwa kuwa mtumizi kwa mujibu wa uwezo wake wa kifedha. Usiwe 
·         bahili na pesa zake (wala  usiwe mfujaji).
·         Unapata malipo kwa matumizi yote unayotumia kwa ajili ya kumkirimu (mkeo) hata kwa kipande kidogo cha mkate ambacho unamlisha kwa  mkono wako  (hadiyth).
·         Unahimizwa  sana kumpa kabla yeye hajakuomba.


10.    Kunukia vizuri na kujipamba mwili

·         Kufuata Sunnah ya kunyoa nywele za  utupuni na   kwapani.
·         Daima uwe msafi na nadhifu.
·         Jitie manukato kwa ajili yake (mkeo)


11.    Jimai (Tendo la ndoa)

·         Unawajibika kulifanya mara kwa mara iwapo huna dharura (ugonjwa,n.k)
·         Uanze kwa “BismiLlaah” na du'aa zilizo sahihi.
·         Umuingilie katika sehemu iliyo sahihi tu (sio sehemu ya nyuma)
·         Uanze kwa vitangulizi (vya jimai) ikiwa ni pamoja na maneno ya mapenzi.
·         Uendelee mpaka umtosheleze hamu yake.
·         Mpumzike na mfanyiane mzaha mnapomaliza
·         Epukana na jimai wakati wa damu ya mwezi kwa sababu kufanya hivyo ni haraam
·         Fanya chochote unachoweza kuepuka kuharibu kiwango chake cha haya alicho nacho (haya na staha) mfano kuvua nguo pamoja badili ya kumtaka avue yeye mwanzo huku ukiwa unamuangalia.
·         Epuka wakati wa jimai mkao ambao unaweza kumuumiza mfano kumgandamiza katika kifua inayopelekea kumzuilia pumzi, hususan iwapo wewe  ni mzito.
·         Chagua muda muwafaka kwa jimai na uwe unamjali kwani wakati mwengine anaweza kuwa ni mgonjwa au amechoka.


12.                  Kudhibiti Siri

·         Jiepushe na kutoa habari za siri mfano wa siri za  chumbani, matatizo yake binafsi na masuala mengine  ya kibinafsi.


13.                  Kumuongoza katika kumtii Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)   


·         Muamshe katika sehemu ya tatu ya mwisho ya usiku kusali “Qiyaam-ul-Layl” (Swalah za ziada za usiku zenye sujuud na ruku’u za muda mrefu).
·         Mfundishe kile unachokijua katika Qur-aan na tafsiri zake.
·         Mfundishe “Dhikr” (njia za kumtaja Allaah kama alivyofundisha Mtume) za asubuhi na jioni.
·         Muhimize kutumia pesa kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kama vile kutoa sadaka.
·         Mchukue katika safari ya Hijja na 'Umrah wakati unapokuwa na uwezo.


14.    Kuonyesha heshima kwa familia yake na rafiki zake

·         Mchukue katika matembezi kwa familia na jamaa, hususan wazazi wake.
·         Waalike kumtembelea na wakaribishe.
·         Wapatie zawadi kunapokuwa na jambo maalum (kama sikukuu)
·         Wasaidie wanapokuwa na haja kwa msaada wa fedha, nguvu, n.k.
·         Endeleza uhusiano mzuri na familia yake baada ya kifo  chake iwapo atakufa mwanzo. Pia kwa hali kama hii mume anahimizwa kufuata Sunnah na kutoa kile ambacho yeye (mke) alizoea kutoa wakati wa uhai wake kuwapa rafiki ya jamaa zake.


14.                  Mafunzo ya Kiislam na kumshauri kwa kumrekebisha


            Hii ni pamoja na:
·         Misingi ya Uislam.
·         Haki na wajibu wake.
·         Kusoma na kuandika.
·         Kumhimiza kuhudhuria darsa na halaqah(darsa duara za Msikitini na majumbani).
·         Hukumu za Kiislam zinazowahusu wanawake.
·         Kumnunulia vitabu vya Kiislam na kaseti kwa ajili ya maktaba ya nyumbani.



16.       Wivu unaokubalika
·         Hakikisha kuwa anavaa hijaab kamili anapotoka  nyumbani.
·         Usimruhusu kuchanganyika ovyo na wanaume  wasio- Mahram.
·         Jiepushe na wivu uliozidi mno. Mfano wake ni kama:

1.      Kulichambua kila neno na sentensi asemayo  na kuyajaza maneno yake kwa maana ambazo hakuzikusudia.
2.      Kumzuia kutoka nje ya nyumba hata kama kuna sababu zinazokubalika.
3.      Kumzuilia kujibu simu, n.k.


17.    Subira na Upole

·        Matatizo yanatarajiwa katika kila ndoa kwa hivyo hili ni jambo la kawaida, Lililo kosa ni majibizano ya kupindukia na kuyakuza matatizo mpaka yakapelekea kuvunjika kwa ndoa.
·         Hasira lazima zionyeshwe pale anapochupa mipaka ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), kwa kuchelewesha Swalah, kusengenya, kuangalia yasiyofaa katika TV, n.k.
·         Kumsamehe makosa anayokukosea wewe  (Angalia sehemu ya 18).
·         Ni namna gani unaweza kumrekebisha makosa yake?


1-   Kwanza, mpe ushauri kwa njia ya mzunguko na ya moja kwa moja mara kwa mara
 2-   Kisha kwa kumpa mgongo katika kitanda kumuonyesha hisia zako). Tanabahi kuwa hii  haihusishi kuhamia chumba kingine, kuhamia  nyumba nyingine, au kutomsemesha


3-   Utatuzi  wa mwisho ni kumpiga kidogo (kwa namna ilivyoruhusiwa) Katika hali hii, mume ni lazima aangalie yafuatayo

·        Ni lazima ujue kuwa Sunnah ni kuepukakumpiga kwani Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakuwahi kumpiga mwanamke wala mtumwa

·        Ni lazima ufanye hivyo katika hali ya juu kabisa ya kutotii, mfano mara kwa mara kukataa tendo la jimai bila ya sababu, mara kwa mara kutosali kwa wakati wake, kuondoka nyumbani kwa muda mrefu bila ya ruhusa na kukataa kusema pahala alipokuwepo, n.k

·        Usifanye hivyo mpaka awe umeshampa  mgomo na kulijadili hilo suala pamoja nae kama ilivyoelezwa katika Qur-aan

·        Usimpige pigo la nguvu la kumuumiza  au  kumpiga usoni au katika sehemu zilizo   nyepesi kuathirika katika mwili wake.


      ·        Jiepushe na kumdhalilisha kama kumpiga kwa kiatu, n.k.


18.    Kusamehe na makaripio yanayofaa

 ·        Mhukumu kwa makosa makubwa tu
 ·        Msamehe makosa aliyokukosea wewe bali mhukumu kwa makosa ya haki za Allaah, mfano kuchelewesha Swalah,  n.k
 ·        Kumbuka mazuri yote anayomfanyia kila wakati  anapofanya makosa
 ·        Kumbuka kuwa kila mwanaadamu hukosea na umuwazie dharura mfano huenda amechoka, ana huzuni, yumo katika siku zake za mwezi au imani/mafungamano yake katika Uislam bado yamo katika kukua   

 ·        Jiepushe na kumgombeza  kwa mapishi mabaya kwani Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakuwahi kumlaumu yeyote katika wake zake kwa jambo hili. Iwapo amekipenda chakula, hula na iwapo hakukupenda hukiwacha na  hatoi maoni yoyote.
 ·        Kabla ya kumuwekea wazi kuwa amefanya makosa, jaribu njia nyingine za mzunguko ambazo ni za hekima kuliko kumlaumu wazi wazi
 ·        Epukana na kutumia jeuri au maneno yanayoumiza hisia zake
 ·        Inapokuwa kuna ulazima wa kujadili tatizo subiri mpaka mnapokuwa faragha
 ·        Subiri mpaka hasira zipungue kidogo, hii inasaidia kuweza kudhibiti maneno yako

KUMSALIA MAITI

Kumsalia maiti ni wajibu kwa Waislamu wote waliohudhuria na sio kwa mtu mmoja mmoja, kwa kiasi kwamba wakiitekeleza wanaotosheleza, walio baki wanakuwa hawana dhambi. Mtume, swallahlahu alayhi wasalam, amempa habari njema mwenye kumsalia maiti kwamba atapata malipo makubwa yanayolingana na mlima. Amesema: «Mwenye kuhudhuria Jeneza hadi akaswali, atapata Kirati, na mwenye kuhudhuria mpaka marehemu akazikwa atapata Kirati mbili. Mtume aliulizwa: Na Kirati mbili ni nini?  Alijibu: Ni mfano wa milima miwili mikubwa».  (Bukhari, Hadithi Na. 1325. Muslim, Hadithi Na. 945) .


Namna Ya kumswalia maiti


Namna yake ni kwamba maiti huwekwa mbele kati ya anayeswali na kati ya Kibla. Mwenye kuswali anasimama mbele ya kichwa cha mwanaume, na kwa mwanamke ansimama katikati yake, kama ilivyo nukuliwa kwa Mtume, swallahlahu alayhi wasalam. (Abudaud, Hadithi Na. 3196)


Inapendekezwa swala ya maiti ifanyike kwa Jamaa, na Imamu awe mbele ya maamuma, kama ilivyo kawaida katika swala ya Jamaa.


Mwenye kuswalia maiti ataleta Takbira nne kama ifuatavyo:


Takbira ya kwanza: Atasoma suratil Fatiha baada yake.




Takbira ya pili: Atamsalia Mtume baada yake kwa kutumia aina yoyote ya matamshi kama kusema:(Allaahumma Swalli wasallim Alaa Nabiyyinaa Muhammad = Ewe Mola wangu, mswalie na mdumishie amani Mtume wetu Muhammad. Kama atamswalia Mtume kikamilifu kama ambayo mwenye kuswali anasema katika Tashahudi ya Mwisho katika swala, inakuwa jambo kamilifu zaidi. Namna ya kumswalia Mtume kikamilifu ni hivi: (Allaahumma Swalli Alaa Muhammad. Wa Alaa Aaali Muhammad. Kamaa Swallaita Alaa Ibraahiim Wa Alaa Aali Ibraahiim. Innaka Hamiidun Majiid. Wabaarik Alaa Muhammad Wa Alaa Aali Muhammad. Kamaa Baarakta Alaa Ibraahiim Wa Alaa Aali Ibraahiim. Innaka Hamiidun Majiid = Ewe Mola wangu, mfikishie rehema Muhammad na familia ya Muhammad, kama ulivyomfikishia rehema Ibrahim na familia ya Ibrahim. Kwa yakini, wewe ni mwenye kusifika, mtukufu. Ewe Mola wangu, mbariki Muhammad na familia ya Muhammad, kama ulivyo mbariki Ibrahim na familia ya Ibrahim. Kwa yakini, wewe ni mwenye kusifika, mtukufu).


Takbira ya tatu: Baada yake atamuombea maiti rehema, msamaha, pepo na kunyanyuliwa daraja kwa yale ambayo Allah atayafungua katika ulimi wake na moyo wake. Kama mwenye kuswali anahifadhi baadhi ya dua zilizopokewa kwa Mtume kuhusu swala ya maiti itakuwa bora zaidi kuomba kwa kutumia dua hizo. Miongoni mwa dua hizo ni hizi zifuatazo: «Allaahummagh-firlahuu Warhamhu. Wa-aafihii Wa’fu Anhu. Wa-akrim Nuzulahuu. Wawassi’mudkhalahuu. Wagh-silhu Bilmaa’i wath-thalji Walbaradi. Wanaq-qihii minal-khatwaayaa Kamaa yunaq-qath-thaubul-abyadhwu Minad-danas. Wa-abdilhu Daaran Khairan Min-daarihii. Wa-ahlan Khairan Min-ahlihii. Wazaujan Khairan Min-zaujihii. Wa-ad-khilhul-jannah. Wa-aidh-hu Min-adhaabil-qabri au min-adhaabin-naar» (Ewe Mola wangu,  msamehe na mrehemu. Na muepushie mabaya  na msamehe. Na ukirimu ujio wake, na mpanulie makao yake na muoshe kwa maji na theluji na barafu na msafishe asiwe na madhambi kama nguo nyeupe inavyo safishwa ikawa haina uchafu. Na mbadilishie nyumba bora zaidi kuliko nyumba yake, na familia bora zaidi kuliko familia yake, na mke bora zaidi kuliko mkewe, na muingize peponi, na mkinge asipate adhabu ya kaburini au adhabu ya motoni.) (Muslim, Hadithi Na. 963)


Takbira ya nne: Baada yake atakaa kimya kidogo, kisha atatoa salamu upande wake wa kulia na wa kushoto, au upande wake wa kulia. Yote hayo yamethibiti kunukuliwa kwa Mtume, swallahlahu alayhi wasalam.


Sehemu ya kuswalia swala ya jeneza


Swala ya Jeneza inafaa kuswaliwa msikitini, au katika sehemu maalumu iliyoandaliwa nje ya msikiti kwa ajili hiyo, na pia inafaa kuswaliwa makaburini. Yote hayo yamethibiti kupokewa kwa Mtume, swallahlahu alayhi wasalam.




Mtume ametoa habari njema kwamba mazishi yana malipo makubwa.  

Friday 26 February 2016

Staa wa muziki Mzungu Kichaa Awadiss Wema Sepetu na Idris Sultan


Staa wa muziki Mzungu Kichaa, amevunja
ukimya kuligusia suala ambalo pengine
linawaumiza wasanii wengi, ikionekana
kuwa ni 'diss' pia kwa staa Wema Sepetu
na mwenzake Idriss Sultan, kupitia suala
lao la ujauzito kunasa na kutoka.
Akiongea kwa hisia nzito, Mzungu Kichaa
ambaye ana project kubwa ya video
ambayo watu hawaifahamu kama
wanavyofahamu mimba ya Wema, msanii
huyo anayejinadi kuwa ni mbishi,
ameelezea kusikitishwa kwake kwa
mastaa hao ambao wanatumia muda wao
mwingi kuleta atensheni kwa mashabiki
badala kufanya shughuli zao binafsi za
kila siku.
Mzungu Kichaa pia amekanusha suala la
video yake kukosa kiki kutokana na
kumhusisha Dir Adam Juma ndani yake,
na kuifanyia hapa hapa nchini akisema
kuwa Dir Adam ana kila


Majina Ya Mawaziri MAJIPU Yakabidhiwa Kwa Waziri Mkuu......Ni Wale Waliogoma Kutangaza Mali Zao

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imemkabidhi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa majina ya baadhi ya mawaziri na naibu mawaziri ambao hawajajaza fomu za mali wanazozimiliki kama sheria inavyowataka.

Akizungumza jana kwenye semina ya mawaziri na naibu mawaziri, Kamishina wa Sekretarieti hiyo, Jaji mstaafu Salome Kaganda alisema viongozi hao wanajua umuhimu wake lakini wanapuuza.

“Sheria hii ya Maadili ya Viongozi wa Umma inajulikana, lakini jambo la kushangaza wapo baadhi ya mawaziri na manaibu ambao hawajajaza, kwa ruhusa yako nitakukabidhi majina yao, sisi tunafanya kazi kwa mujibu wa sheria, hivyo anayekiuka anapaswa kuadhibiwa,” alisema Jaji Kaganda bila kutaja majina hayo.

Kifungu cha 9 cha sheria hiyo kinataka katika kipindi cha siku 30 baada ya kupewa wadhifa, kila mwisho wa mwaka na mwisho wa kutumikia wadhifa wake kiongozi husika anatakiwa kupeleka tamko la maandishi la mali zake.

Sheria hiyo inafafanua kuwa mali hizo ni pamoja na rasilimali zake au mume au watoto wenye umri usiozidi miaka 18 ambao hawajaoa au kuolewa.

Alisema fomu hizo lazima zijazwe na viongozi na wananchi wanaruhusiwa kwenda kuzihakiki wakitoa sababu za msingi, lakini sheria hiyo hairuhusu waende kutangaza na wakifanya hivyo hatua zinachukuliwa dhidi yao.

“Hapo ndipo wananchi wengi huwa hawatuelewi kwa kuwa wanapenda kujua mali ambazo viongozi wao wanamiliki,” alisema.

Alisema Sekretarieti kwa kutambua umuhimu wa viongozi hao kuzingatia sheria na maadili, ndiyo sababu imeandaa semina hiyo baada ya kupata ufadhili kutoka Shirika la Misaada ya Maendeleo la Marekani (USAID), wakiamini kuwa yatasaidia kuwakumbusha.

Ester Bulaya Atamba 'Nitaendelea Kumgaragaza Wasira Ubunge wangu si Wakuchakachua'


Mbunge wa Bunda Mjini, mkoani Mara, Esther Bulaya (Chadema), ametamba kuwa ataendelea kumshinda mpinzani wake kisiasa, Stephen Wasira (CCM), kwa madai kwamba alipata ubunge huo kihalali.

Bulaya alisema hayo jana ikiwa ni siku moja tangu kutupwa kwa rufaa ya wanachama wa CCM waliokuwa wakipinga ushindi wa mbunge huyo alioupata katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 dhidi ya Wassira na wagombea wa vyama vingine.

Mbunge huyo aliiambia Nipashe kwa njia ya simu kutoka jimboni kwake kuwa, alimshinda Wasira kwa wananchi, akamshinda kisheria, lakini hakuridhika akakata rufaa na ameendelea kumshinda.

"Kama ana mpango wa kukata rufaa nyingine aende akate tu, lakini akumbuke kuwa nitaendelea kumshinda tu kwa sababu ubunge wangu sio wa kuchakachua bali nimeupata kutokana na kura za wananchi wa Bunda Mjini," alisema Bulaya na kuongeza:

"Siku zote nimekuwa nikisema kuwa waliofungua kesi sio wanachama wa CCM bali ni Wasira mwenyewe, ndio maana akawa mkali kupigwa picha na waandishi ili Watanzania waendelee kudhani kwamba hayumo katika kesi hiyo," alisema.

Alisema wakati umefika sasa mwana siasa huyo mkongwe kupumzika na kula mafao yake, kwa kile alichosema ametumikia taifa kwa muda mrefu na sasa ni zamu ya wengine kumpokea kijiti ili kuanzia pale alipoachia.

"Pamoja na hayo ninamkumbusha kuwa siku zote mahakama husimamia haki ndio maana ameshindwa mara mbili katika kesi hii, hivyo hana budi kupumzika," alisema.

Januari 25 mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilitupilia mbali kesi ya uchaguzi iliyofunguliwa na wapigakura Magambo Masato, Matwiga Matwiga, Janes Ezekiel na Ascetic Malagira kupinga ubunge wa Bulaya.

Bulaya alihama CCM na kujiunga na Chadema katikati ya mwaka jana na kuteuliwa na Chadema kuwania ubunge wa Jimbo la Bunda Mjini na kufanikiwa kumbwaga mkongwe huyo kwenye Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana