Friday 21 August 2015

Kanisa Katoliki limemzuia staa wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel kumbatiza mwanaye kutokana na...........

 Kanisa Katoliki limemzuia staa wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel kumbatiza mwanayekutokana na kutokidhi matakwa ya kanisa.

Tukio hilo limetokea hivi karibuni mara baada ya mwigizaji huyo ambaye imani yake ni ya Kiislamu, kutaka kumbatiza mwanaye huyo ambaye baba yake ( Moze Iyobo) ni Mkatoliki.

“Alikuwa amejipanga kumbatiza Kikristo kutokana na imani ya baba mtoto wake lakini alipokutana na padri Paul Ruwaaich wa Parokia ya Uparo Moshi aliyekuwa Dar kikazi akamtaka akaanzie kusali kwenye Jumuiya Ndogondogo (mtaani kwake), abadilishe dini ndipo mtoto huyo abatizwe kwani ndizo taratibu za Kanisa Katoliki.

“Alipopewa sharti hilo, lilikuwa gumu kwa Aunt, ikabisi ageuze zake,” kilisema chanzo chetu.

Mwanahabari wetu alipomuuliza Aunt kuhusu suala hilo, alisema amebaki njia panda na anatafakari cha kufanya

0 comments:

Post a Comment