Showing posts with label Habar. Show all posts
Showing posts with label Habar. Show all posts

Monday, 17 September 2018

🌹ADABU YA MUME KWA MKEWE.🌹


Usitangaze udhaifu wa mkeo kwa familia na marafiki, kila mmoja anamtunzia mwenziwe hadhi yake.

Usiwe na mtizamo mbaya wala kuzungumza naye kwa hisia kali huwezi kujua atatafsiri vipi.!!

Usimlinganishe mkeo na wanawake wengine, huwezi kujua hao wanawake wengine wanapitia hali gani kimaisha, kila mwanamke anasifa zake.

Usisahau kwamba ni mkeo umemuoa, yeye si kijakazi, muhudumie kama malikia na atauonyesha ulimwengu kwamba Mumewe ni mfalme na utamtawala maishani.

Mpe kipaumbele na ni wajibu wako binafsi kumfanyia jambo na sio watuwengine.

Usimlaumu mbele za watu hata kama kakosea, mlinde, muhimize, mrekebishe faraghani, ukifanya hivyo kamwe hatokusahau.

Usimnyime huduma za kitandani kwa kujifanya mgonjwa/kuchoka ama kutokuwa na hamu, kumbuka wanaume wengine wanatafuta nafasi hiyo.

Usimlinganishe mkeo na mtalaka wako ama mkeo aliyefariki maana wewe ni mume wa pekee kwake.

Usimkemee wala kumkosoa mbele ya watoto, ni malezi mabaya kwa watoto maana wewe ni mwalimu wao, wanakutazama wewe japo unadhani ni watoto tu!!.

Mtazame mkeo kama kavaa vizuri kabla hajatoka maana akipendeza yeye na wewe unaheshimika na ukipendeza wewe yeye anaheshimika.

Usikubali marafiki kuwa karibu na mkeo, weka mipaka maana hujui nia zao.

Usitoke kuoga na haraka haraka ukavaa nguo ukatoka pasi yeye kukukagua, mkeo kazungukwa na wanaume wanadhifu wanaojali mavazi na utanashati.

Wazazi, ukoo na marafiki sio waamuzi kwa mambo ya mkeo, usipoteze muda kutafuta uamuzi wa mwisho kutoka kwao, ithibiti ndoa yako.

Mapenzi yako yasiwe kwa sababu ya mazingira au kihali hata kama ulimuoa kwa misingi hiyo kwa sasa ni mkeo mpende bila masharti, hali uweza kubadilika na ikiwa ndio msingi basi ndoa itavunjika.

Mkeo anahitaji umakinike kwake na umsikilize kama mtoto, usiwe mkali msikilize kwa makini na atakupenda.

Usijilinganishe na mkeo, yeye ni mke kwa hivyo msaidie tu maanandoa ni kusaidia.

Usimuhukumu mkeo, ni msaidizi wako na kiumbe dhaifu mchukulie kwa mtazamo huo na utapata utulivu wa akili.

Mume mzembe hajali, haogi, jiweke nadhifu ukiwa na yeye nukia vizuri, harufu mbaya inamkirihisha ila hawezi kukwambia.

Usiwe na urafiki na waume walio na mtazamo mbaya kuhusu ndoa. Watakuharibu mawazo.

Mkeo ana thamani kubwa sana ndio maaana ukatoa vitu vya thamani kumuoa, penzi lenu lifanye jipya, uzembe haufai.

Kuzaa ni majaaliwa, mpende mkeo awe na watoto au asiwe nao, usiwabague watoto kwa jinsia wafunze dini na watakuwa wacha Mungu hadi maishani mwao.

Hauwi mzee kwa mkeo katika kumburudisha, usiwe na ugomvi naye mutakuwa katika kheri, usiwache kuwajali watoto wako na mkeo kwa sababu ya wanawake wengine au sababu yoyote ile, wao ni wewe na wewe ni wao.

Mume anayedumu na ibada ana usalama, omba kila siku, muombee mkeo na watoto.

Ukijiunga na group letu la UISLAMU CHAGUO LANGU na kulike page yetu ya Habari za kiislamu na kututembelea Furaha ya Ndoa utaelimika na ndoa yako.

💕TUKIYAFANYA HAYA TUTAKUWA NA NDOA BORA MNO!!💕

KUMSALIA MAITI

Kumsalia maiti ni wajibu kwa Waislamu wote waliohudhuria na sio kwa mtu mmoja mmoja, kwa kiasi kwamba wakiitekeleza wanaotosheleza, walio baki wanakuwa hawana dhambi. Mtume, swallahlahu alayhi wasalam, amempa habari njema mwenye kumsalia maiti kwamba atapata malipo makubwa yanayolingana na mlima. Amesema: «Mwenye kuhudhuria Jeneza hadi akaswali, atapata Kirati, na mwenye kuhudhuria mpaka marehemu akazikwa atapata Kirati mbili. Mtume aliulizwa: Na Kirati mbili ni nini?  Alijibu: Ni mfano wa milima miwili mikubwa».  (Bukhari, Hadithi Na. 1325. Muslim, Hadithi Na. 945) .


Namna Ya kumswalia maiti


Namna yake ni kwamba maiti huwekwa mbele kati ya anayeswali na kati ya Kibla. Mwenye kuswali anasimama mbele ya kichwa cha mwanaume, na kwa mwanamke ansimama katikati yake, kama ilivyo nukuliwa kwa Mtume, swallahlahu alayhi wasalam. (Abudaud, Hadithi Na. 3196)


Inapendekezwa swala ya maiti ifanyike kwa Jamaa, na Imamu awe mbele ya maamuma, kama ilivyo kawaida katika swala ya Jamaa.


Mwenye kuswalia maiti ataleta Takbira nne kama ifuatavyo:


Takbira ya kwanza: Atasoma suratil Fatiha baada yake.




Takbira ya pili: Atamsalia Mtume baada yake kwa kutumia aina yoyote ya matamshi kama kusema:(Allaahumma Swalli wasallim Alaa Nabiyyinaa Muhammad = Ewe Mola wangu, mswalie na mdumishie amani Mtume wetu Muhammad. Kama atamswalia Mtume kikamilifu kama ambayo mwenye kuswali anasema katika Tashahudi ya Mwisho katika swala, inakuwa jambo kamilifu zaidi. Namna ya kumswalia Mtume kikamilifu ni hivi: (Allaahumma Swalli Alaa Muhammad. Wa Alaa Aaali Muhammad. Kamaa Swallaita Alaa Ibraahiim Wa Alaa Aali Ibraahiim. Innaka Hamiidun Majiid. Wabaarik Alaa Muhammad Wa Alaa Aali Muhammad. Kamaa Baarakta Alaa Ibraahiim Wa Alaa Aali Ibraahiim. Innaka Hamiidun Majiid = Ewe Mola wangu, mfikishie rehema Muhammad na familia ya Muhammad, kama ulivyomfikishia rehema Ibrahim na familia ya Ibrahim. Kwa yakini, wewe ni mwenye kusifika, mtukufu. Ewe Mola wangu, mbariki Muhammad na familia ya Muhammad, kama ulivyo mbariki Ibrahim na familia ya Ibrahim. Kwa yakini, wewe ni mwenye kusifika, mtukufu).


Takbira ya tatu: Baada yake atamuombea maiti rehema, msamaha, pepo na kunyanyuliwa daraja kwa yale ambayo Allah atayafungua katika ulimi wake na moyo wake. Kama mwenye kuswali anahifadhi baadhi ya dua zilizopokewa kwa Mtume kuhusu swala ya maiti itakuwa bora zaidi kuomba kwa kutumia dua hizo. Miongoni mwa dua hizo ni hizi zifuatazo: «Allaahummagh-firlahuu Warhamhu. Wa-aafihii Wa’fu Anhu. Wa-akrim Nuzulahuu. Wawassi’mudkhalahuu. Wagh-silhu Bilmaa’i wath-thalji Walbaradi. Wanaq-qihii minal-khatwaayaa Kamaa yunaq-qath-thaubul-abyadhwu Minad-danas. Wa-abdilhu Daaran Khairan Min-daarihii. Wa-ahlan Khairan Min-ahlihii. Wazaujan Khairan Min-zaujihii. Wa-ad-khilhul-jannah. Wa-aidh-hu Min-adhaabil-qabri au min-adhaabin-naar» (Ewe Mola wangu,  msamehe na mrehemu. Na muepushie mabaya  na msamehe. Na ukirimu ujio wake, na mpanulie makao yake na muoshe kwa maji na theluji na barafu na msafishe asiwe na madhambi kama nguo nyeupe inavyo safishwa ikawa haina uchafu. Na mbadilishie nyumba bora zaidi kuliko nyumba yake, na familia bora zaidi kuliko familia yake, na mke bora zaidi kuliko mkewe, na muingize peponi, na mkinge asipate adhabu ya kaburini au adhabu ya motoni.) (Muslim, Hadithi Na. 963)


Takbira ya nne: Baada yake atakaa kimya kidogo, kisha atatoa salamu upande wake wa kulia na wa kushoto, au upande wake wa kulia. Yote hayo yamethibiti kunukuliwa kwa Mtume, swallahlahu alayhi wasalam.


Sehemu ya kuswalia swala ya jeneza


Swala ya Jeneza inafaa kuswaliwa msikitini, au katika sehemu maalumu iliyoandaliwa nje ya msikiti kwa ajili hiyo, na pia inafaa kuswaliwa makaburini. Yote hayo yamethibiti kupokewa kwa Mtume, swallahlahu alayhi wasalam.




Mtume ametoa habari njema kwamba mazishi yana malipo makubwa.