Friday 7 August 2015

MAALIM SEIF SHARIFF HAMAD:Haya ndio maneno yake baada ya Prof lipumba kuondoka cuf

Katibu mkuu wa chama cha Wanachi CUF nchini Tanzania Maalim Seif Shariff Hamad amewaambia wafuasi wa chama hicho kuwa chama hakitayumba kutokana na kuondoka kwa aliekuwa mwenyekiti wa chama hicho profesa Ibrahimu lipumba. Maalim Seif ameongea na wafuasi wa chama hicho hayo majira ya usiku baada ya wafuasi hao kukaa nje ya makao makuu ya chama hicho kwa zaidi ya saa nane wakisubiri kusikia kauli ya kiongozi huyo ambae aliwasili kutoka zanzibar majira ya saa mbili usiku

0 comments:

Post a Comment